Thursday, November 9, 2017

Tiba mbadala ya uzazi wa mpango

Tiba mbadala ya uzazi wa mpango


1. Papai
Mbegu za Papai pia ni dawa nzuri ya uzazi wa mpango kwa upande wa wanaume. Zinachofanya mbegu za papai ni kupunguza idadi ya uwingi wa mbegu za mwanaume (sperm count) na zinaweza kushuka mpaka kufika sifuri (zero sperm count) na hivyo mwanaume anakuwa hana uwezo wa kutungisha mimba. Ukihitaji kuzaa tena unaacha tu kuzitumia na hali yako itarudi kama kawaida. Kula mbegu za papai kijiko kidogo kimoja cha chai kutwa mara 1 kila siku.
Unaweza kuanza zoezi hili wiki 3 kabla hujaamua rasmi kama ndiyo dawa yako ya uzazi wa mpango.
Watu wa bara la Asia wamekuwa wakitumia mbinu hii tangu miaka mingi iliyopita. Dawa hii haina madhara yoyote.
2. Mbegu za Nyonyo
Watafiti katika chuo kikuu cha Kano State College of Arts, Science and Remedial Studies cha Nigeria wamethibitisha kuwa mbegu za nyonyo zinaweza kutumika kama dawa ya uzazi wa mpango. Mbegu za nyonyo zinatumika kwa miaka mingi nchini India kama dawa ya uzazi wa mpango.
Unachotakiwa kufanya ni kunywa na maji mbegu 4 mpaka 5 kwa siku kila siku wakati wa siku zako na zitakupa kinga ya uzazi wa mpango karibu kwa mwaka mzima. Menya ganda lake la nje kabla ya kumeza.
Siku mbili au tatu za mwanzo za kutumia unaweza ukapatwa na kutokujisikia vizuri, pumzi fupi, vipele (rashes), kizunguzungu kidogo, kutapika au kuharisha nk lakini baadaye hali itatulia.
3. Tangawizi
Tangawizi huhamasisha kutokea kwa siku zako. Kunywa vikombe vitatu mpaka vinne vya chai ya tangawizi kila siku ili kuzuia ujauzito. Chota kijiko kidogo kimoja cha chai cha unga wa tangawizi na uweke ndani ya maji ya moto kikombe kimoja (robo lita/ml 250) na unywe yote (unaweza kuongeza asali kidogo kupata ladha). Fanya zoezi hili kutwa mara 3 mpaka mara 4 kwa siku 5 tangu ufanye tendo la ndoa bila kinga. Unaweza pia kutumia tangawizi mbichi kwa matokeo mazuri zaidi.
4. Kotimiri (Parsley):
Kotimiri inapatikana kirahisi Dar Es Salaam na Zanzibar na ni kiungo mhimu kwenye mahoteli mengi ya kitalii. Kunywa kikombe kimoja (robo lita/ml 250) asubuhi na jioni cha chai iliyoandaliwa ukitumia kotimiri mbichi kila siku ili kuzuia ujauzito usiotarajiwa. Hakuna madhara yoyote mabaya ya matumizi ya dawa hii.
5. Vitamin C
Vitamini C ikitumika katika hali yake ya uasili kabisa inaweza kutumika kama dawa ya uzazi wa mpango.  Kwenye vitamini C kuna ‘ascorbic acid’ ambayo huzuia homoni inayouandaa mji wa uzazi (‘progesterone hormone’) kushindwa kufanya kazi zake vizuri na hivyo mimba kukosa mahali pa kukaa baada ya yai kurutubishwa.
Meza viponge vya vitamini C mg 1500 mara mbili kwa siku mbili mpaka tatu baada kushiriki tendo la ndoa bila kinga. Vitamin C ni nzuri pia kwa ngozi yako.
Mhimu:
1) Usitumie kiasi kingi sana cha vitamini C kwani inaweza kupelekea mwili wako kutokuwa sawa au unaweza usijisikie vizuri katika mwili wako.
2) Usitumie vitamini C kama unatumia dawa za kuzuia damu kuganda (anti-coagulant medications).
3) Usitumie vitamini C kama una tatizo la sickle cell (sikoseli).
Kumbuka kuwa makini mara zote, na wewe fanya utafiti binafsi pia.

Toa maoni yako.

No comments:

Post a Comment